Thursday 10 August 2017

LWANDAMINA AFUTA MASALIA YA SIMBA YANGA


Mshambuliaji wa Yanga, Ibrahim Ajibu ataanza kuonekana akicheza tofauti na ilivyokuwa Simba hasa katika wakati wa ushambulizi, pia kukaba.

Kocha George Lwandamina ameyasoma mapungufu ya Ajibu wakati akiwa Simba na taratibu amekuwa akiyafanyia kazi mapungufu hayo.

“Unajua Ajibu alikuwa hakabi, lakini pia uchezaji wake licha ya kuwa na kipaji, kocha aliona haukuwa ule wa malengo sana,” kilieleza chanzo ndani ya Yanga.

“Utaona kama vile anakaa na mpira muda mrefu bila sababu au kucheza na jukwaa. Lakini kocha amemueleza kuwa ni lazima kufanya kazi kwa malengo kwa kuwa dakika 90 ni chache sana lazima kuzitumia vizuri.”

Kweli mara kadhaa, Lwandamina ameonekana kufanya mazoezi na Ajibu akimsisitiza masuala kadhaa akionyesha amepania kumrekebisha.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive