Tuesday 25 July 2017

YANGA YAMSAJILI KIPA WA SERENGETI BOY


Ramadhani Kabwili.
Baada ya tetesi ndani ya wiki kadhaa, hatimaye Klabu ya Yanga imesajili kipa chipukizi, Ramadhani Kabwili.
Kipa huyo aliyekuwa akiidakia timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys amesaini mkataba wa miaka mitano kuitumikia klabu hiyo yenye makao makuu mitaa ya Jangwani jijini Dar es Salaam.
Kabwili anaungana na kipa mwingine mpya, Mcameroon Youthe Rostand aliyesajiliwa kutoka African Lyon na Benno Kakolanya ambaye huu utakuwa msimu wa pili tangu asajiliwe akitokea Tanzania Prisons ya Mbeya.
Kabwili na Rostand wote wanasajiliwa kuchukua nafasi za makipa wa muda mrefu wa Yanga, Ally Mustafa ‘Barthez’ na Deogratius Munishi ‘Dida’ waliomaliza mikataba yao na kuruhusiwa kuondoka.
Share:

1 comment:

Ads

Blog Archive