Monday 10 July 2017

RASMI MWAKYEMBE AVUNJA BARAZA LA MICHEZO


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe leo Julai 10 amesitisha uteuzi wa mwenyekiti pamoja na wajumbe wote wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT) kuanzia leo kwa mamlaka aliyopewa na sheria ya BMT Na.12 ya 1967.

Mwakyembe ameeleza kuwa sababu ya kusitisha uteuzi huo inatokana na agizo alilopewa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliyemwagiza afanyie kazi mapitio na kulitathmini upya baraza hilo ili kujiridhisha na usimamizi wake kuhusu michezo.

Kutokana na kujiridhisha kwake kwamba usimamizi wa BMT si imara, basi ameweza kulivunja na ataliunda upya na kwa sasa sekretarieti ya balaza hilo itaendelea kufanya kazi katika kipindi hiki ikishirikiana na wizara.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive