Mshambuliaji wa kimataifa wa Simba kutoka Uganda, Emmanuel Okwi, ametua
kambini Afrika Kusini jana na kuwaambia mashabiki wa timu hiyo wajiandae
kuona "vitu vyake" katika mechi ya kirafiki dhidi ya Rayon FC
itakayofanyika Agosti 8 (Simba Day).
Okwi amewaambia mashabiki na wanachama wa Simba wawe watulivu, amejiandaa kuwapa kile wanachokitarajia kutoka kwake na anafahamu vizuri ndoto za klabu hiyo yenye makao makuu yake Mtaa wa Msimbazi, Kariakoo jijini.
"Nitakuwa Dar es Salaam siku ya Simba Day, najua watu wanahamu ya kuniona, mashabiki wawe watulivu," alisema mshambuliaji huyo.
Okwi amewaambia mashabiki na wanachama wa Simba wawe watulivu, amejiandaa kuwapa kile wanachokitarajia kutoka kwake na anafahamu vizuri ndoto za klabu hiyo yenye makao makuu yake Mtaa wa Msimbazi, Kariakoo jijini.
"Nitakuwa Dar es Salaam siku ya Simba Day, najua watu wanahamu ya kuniona, mashabiki wawe watulivu," alisema mshambuliaji huyo.
0 comments:
Post a Comment