Saturday 1 July 2017

KUMEKUCHA KIBITI MAJINA YA WAHALIFU YAZIDI KUBAINIKA



Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Eng. Hamad Yussuf Masauni ametangaza kuwa, Jeshi la Polisi linawasaka watuhumiwa 16 wa mauaji ambayo yamekuwa yakiendelea kufanyika katika maeneo ya Kibiti, Mkuranga na Rufiji Mkoani Pwani kwa muda mrefu sasa.

Baadhi ya majina hayo ni kama yanavyoonekana hapo juu.


Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Masauni amesema kuwa watuhumiwa hao wanafahamika na tayari jeshi la polisi lina picha za watuhumiwa wote ambao wanasakwa.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive