Leo July 20 Mwanasheria, Mbunge wa CHADEMA na Rais wa Chama cha
Mawakili Tanganyika TLS, Tundu Lissu amekamatwa akiwa Airport Dar es
Salaam akielekea Rwanda kwenye mkutano wa Chama cha Mawakili wa Afrika
Mashariki.
Ushindi Media imempata Wakili wake Peter Kibatala na amezungumzia tukio hilo ambapo amesema kuwa ”Mimi
sijaongea naye moja kwa moja kwa sababu simu zake ni ama zimezimika au
zimezimwa lakini taarifa nilizopata kutoka kwa watu wake wakiwemo ambao
wamemuacha Airport muda si mrefu na wengine ninaowaamini ni yes
amekamatwa na anapelekwa Central Police Station.
“Kuna Wakili mwenzangu
anaelekea huko kwenda kushughulikia Haki zake za kisheria na pengine
kusisitiza kwamba apelekwe Mahakamani na sisi kama ni kweli amekamatwa
rai yetu ni hiyo kama wamemkamata na waliomkamata wanaamini kwamba wana
tuhuma dhidi yake wakamilishe taratibu zao mapema kama inavyowezekana
wampeleke Mahakamani tukakutane naye huko.” – Peter Kibatala.
0 comments:
Post a Comment