Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kwamba atapendekeza rasmi kuteuliwa kwa tajiri mmiliki wa klabu inayocheza ligi ya NFL Woody Johnson kuwa balozi wa Marekani nchini Uingereza.
Ni mmiliki wa klabu ya New York Jets ambayo haijakuwa ikifanya vyema Ligi ya Soka ya Taifa (NFL).
Bilionea huyo ni mrithi mtarajiwa wa kampuni kubwa ya dawa ya Johnson & Johnson na amefahamiana na Bw Trump kwa miaka mingi.
Hata
hivyo, Bw Johnson, 70, ambaye alichangia sana juhudi za chama cha
Republican kuchangisha pesa, awali aliunga mkono mpinzani wa Trump
katika mchujo wa chama hicho Jeb Bush.
Amechangia mamilioni ya dola katika mipango na juhudi za chama cha Republican.
Atahitaji kuidhinishwa na bunge la Seneti kabla ya kuchukua rasmi majukumu.
Bw Trump alizua wazo la kumteua kwua balozi mwezi Januari, mkesha wa kuapishwa kwake kuwa rais.
Wadhifa
wa balozi wa Marekani nchini Uingereza umekuwa ukitazamwa na wengi kama
wadhifa mkuu katika diplomasia, na sana huwa unapewa watu wanaochanga
zaidi pesa katika kampeni au washirika wa karibu kisiasa wa utawala.
Waziri Mkuu wa Theresa May amekaribisha uteuzi huo, shirika la habari la Reuters limeripoti.
0 comments:
Post a Comment