SHIRIKISHO la Soka Tanzania
(TFF) kupitia kamati yake ya nidhamu chini ya mwenyekiti wake, Tarimba
Abbas, linatarajia kumjadili beki Juma Nyosso aliyetua Kagera Sugar kwa
ajili ya kuitumikia timu hiyo katika msimu ujao.
Beki huyo alifungiwa na TFF akiwa na
kikosi cha Mbeya City msimu wa 2015/16 kutokana na kosa la kumdhalilisha
mshambuliaji wa Azam FC, John Bocco wakati wa mchezo baina ya timu hizo
mbili.
Kufuatia kukamilisha adhabu yake ya
kufungiwa miaka miwili, Nyosso amefanikiwa kusaini mkataba wa kuitumikia
Kagera Sugar kwa ajili ya msimu ujao wa ligi kuu, hivyo kusababisha TFF
kumjadili. Taarifa ambazo gazeti hili limezipata kutoka TFF ni kuwa
kamati ya nidhamu inatarajia kukutana wakati wowote kuanzia sasa kwa
ajili ya kujadili suala la beki huyo kwa kuwa adhabu yake inafikia
tamati Septemba 20.
“Adhabu ya Nyosso inatarajiwa kufikia
tamati Septemba 20, mwaka huu, hivyo iwapo kamati hiyo itaafi kiana
itamsamehe ili kuweza kumwacha huru aitumikie timu yake mpya,” kilisema
chanzo hicho.
0 comments:
Post a Comment