Thursday 29 June 2017

TETESI ZA USAJILI MAN U, ARSENAL, LIVERPOOL, AC MILLAN, MAN CITY, CHELSEA NA LIVERPOOL



HIZI  HAPA TETESI ZA USAJILI BARANI ULAYA
Arsenal wameambiwa lazima walipe pauni milioni 57 ili kumsajili Alexandre Lacazette, 26, kutoka Lyon (London Evening Standard).
Kinda wa Arsenal Kaylen Hinds anajiandaa kuondoka Emirates na kujiunga na Wolfsburg ya Ujerumani (The Sun).


Mshambuliaji wa Real Madrid Gareth Bale yuko tayari kuondoka Spain na kuhamia Manchester United (Daily Star).
AC Milan wanapanga kutoa kitita kikubwa kumsajili kiungo wa Real Madrid Isco (Don Balon).
AC Milan wanakaribia kumsajili Hakan Calhanoglu kutoka Bayer Leverkusen kwa euro milioni 20 (Sky Sport Italia).

West Brom wanakaribikia kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa Southampton Jay Rodriguez, 27 kwa pauni milioni 12 (Daily Express).
Nahodha wa zamani wa Chelsea John Terry, 36, ameambiwa anaweza kuchukua nafasi ya umeneja wa Aston Villa, iwapo atajiunga na klabu hiyo (Daily Express).


Mchezaji anayenyatiwa na Liverpool Naby Keita, 22, amesema angependa kuchezea moja ya timu kubwa kama vile Barcelona, Real Madrid au Manchester City. Liverpool wanamtaka kiungo huyo wa Red Bull Leipzig (Manchester Evening News).
Beki wa Chelsea Nathan Ake, 22, anakaribia kufanikisha uhamisho wake wa pauni milioni 20 kwenda Bournmouth (Guardian).


Pierre Emerick-Aubameyang, 28, anayenyatiwa na Liverpool anaonekana kukaribia kukamilisha uhamisho wake kwenda Tianjin Quanjian ya China, ambayo imetoa dau la pauni milioni 70 (Daily Star).
Real Madrid bado wanafikiria kuhusu Kylian Mbappe, kwa mujibu wa Rais wa Real, Florentini Perez, ambaye anasema umri wake wa miaka 18 huenda ukawa tatizo katika klabu hiyo ingawa amekiri kuwa Zinedine Zidane yuko karibu na mchezaji huyo na usajili unaweza kufanyika (Independent).
Winga wa Everton Gerard Deulofeu, 23, amekataa nafasi ya kurejea Barcelona, huku AC Milan na Juventus pia zikimtaka (Daily Mail).
Newcastle United wanazungumza na Liverpool kuhusu uhamisho wa mkopo wa winga Sheyi Ojo, 20 (Newcastle Chronicle).
Mkurugenzi mkuu wa Southampton Les Reed amesisitiza kuwa mabeki wake Virgil van Dijk na Cedric Soares hawauzwi. Liverpool na Tottenham zinawataka wachezaji wao (Sky Sports).
Leicester City hawajapokea dau lolote la kumtaka Riyad Mahrez, ambaye amehusishwa na kuhamia Arsenal, Barcelona na Chelsea (Leicester Mercury).
Juventus wanafikiria kumchukua beki wa Real Madrid Danilo, kuziba nafasi ya Dani Alves anayetazamiwa kwenda Manchester City (Corriere dello Sport).
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive