Tuesday 20 June 2017

SABABU YA KUZAA MTOTO MLEMAVU NI HII

Na Denis Massawe

Wanawake wajawazito ambao wana uzito mkubwa au unene uliopitiliza wako hatarini kujifungua watoto wenye ulemavu hasa ulemavu wa miguu kwa mujibu wa Watafiti wa Kisayansi wa Chuo Kikuu cha Stockholm, Sweden.
Utafiti wa Wanasayansi hao umeonesha kuwa tatizo la kuzaa watoto walemavu hutokea iwapo mwanamke huwa mnene kabla ya kutungwa kwa mimba ambapo kwa mujibu wa utafiti huo watoto zaidi 43,550 walizaliwa wakiwa walemavu kutokana na mama zao kuwa wanene.
Mmoja wa watafiti hao Dr. Martina Persson aliiambia Medical Journal kuwa hatari ya watoto kuzaliwa wakiwa walemavu imeongezeka kwa 4.7% huku wengi wao wakizaliwa na ulemavu wa miguu, macho, mikono na matatizo ya moyo.
Akielezea uhusiano uliopo baina ya unene na kuzaliwa kwa watoto walemavu Dr. Raul Artal alisema wanawake wengi ambao ni wanene kupitiliza wana magonjwa kama kisukari na shiniko la damu hivyo hupelekea watoto kutokamilika baadhi ya viungo kutokana na presha ya mwili wa mama mjamzito.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive