Wakati siku zikiendelea kukimbia kama ilivyoada ya mwanamasumbwi mwenye mbwembwe za pesa, Floyd Mayweather ameanza kutamba
kwamba iwe isiwe ni lazima amshinde vibaya mpinzani wake, Conor McGregor
katika pambano lao litakalofanyika Agosti 26, Las Vegas, Nevada nchini
Marekani.
Mayweather ameyasema hayo baada ya kufanya mazoezi kwa saa nne
mfululizo katika gym ya Ten Goose huku akiwa na kundi lake la TMT
akiwemo staa wa NBA, DeMar DeRozan.
“Naweza kuteseka, kufanya mazoezi ya kufa mtu, wakati mwingine mpaka
kubadilika rangi lakini mwisho wa siku nipate kile ninachokitaka
ulingoni. Nitamchakaza sana mpinzani wangu siku hiyo,” alisema
Mayweather kwa mbwembwe.
0 comments:
Post a Comment