Victor Wanyama ameelezea safari yake ya soka tangu alivyoondoka Afrika kwenda Ulaya na baadae kufanikiwa hadi kucheza Tottenham sehemu ambayo anaamini anaweza kutimiza ndoto yake ya kutwaa vikombe kwa sababu yupo kwenye moja ya timu zenye ushindani Duniani.
Wanyama aliondoka Kenya kwenda Ulaya akiwa bado mdogo tofauti na
wengi wanavyofahamu na alikwenda huko kutembea lakini alipopata fursa
akaonesha kipaji chake na hapo ndipo safari rasmi ya soka lake barani
Ulaya ikaanza.
“Mimi nilienda nje nikiwa bado mdogo, nilianzia Sweden halafu
nikaenda Ubelgiji ambako nilikaa sana kama miaka mitano halafu
nikachukuliwa na Celtic lakini ilikuwa ngumu kupata kibali cha kufanyia
kazi ilikuwa ni ngumu kwa sababu rank za Kenya hazikuwa poa zilikuwa
hazijavuka kiwango kinachotakiwa lakini nilikuwa nina miaka 18 kwa hiyo
nikapata bahati ya kuchukuliwa kama special talent nikafanikiwa
kuingia.”
“Ndugu yangu Mariga alikuwa Sweden kwa hiyo mimi nilienda kama
kutembea kufika kule akaenda kuuliza kwenye klabu yake kama naweza
kufanya mazoezi, wakakubali niende nikafanye nao mazoezi nikaenda
wakanipenda wakataka niendelee kuwa nao.”
“Mariga akapata deal Italy kwenye klabu ya Parma nikamuomba twende
pamoja akakataa akaniambia lazima kila mtu awe na njia yake na hapo ndio
nitakomaa kimpira, nikakubaliana nae.”
“Tukapata tournament huko Sweden tukacheza na timu kutoka Ubelgiji na
kulikuwa na scout kutoka Kenya akaniona hapo halafu akaniambia nirudi
Kenya, nikarudi nikafanya nao mazoezi kwa miezi mitatu akanipeleka
Ubelgiji.”
“Spurs nimefika na kuna vitu inabidi nivikamilishe, ndoto yangu
imekuwa ni kushinda vikombe na kwa sasa nimepata klabu ambayo naweza
kutimiza nayo malengo yangu ya kushinda vikombe halafu badae tutaona.”
0 comments:
Post a Comment