WAZIRI Mkuu Mstaafu na mgombea urais mwaka 2015 kwa tiketi ya
Chadema, Edward Lowassa, amewasili katika Makao Makuu ya Polisi jijini
Dar saa nne kama alivyotakiwa na Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai
(DCI).
Lowassa alikuwa amefuatana na magari manne ya msafara wake pamoja na magari mawili ya polisi wenye silaha.
Kabla ya kuwasili kwa Lowassa, aliyetangulia mapema leo alikuwa
katibu Mkuu wa CHADEMA Dkt. Mashinji aliyewasili kuhakikisha anaweka
sawa maswala ya kisheria na msaada wowote utakaohitajika.
Waandishi wa habari hawakuruhusiwa kusogea eneo la tukio kwani ulinzi umeimarishwa.
Jana Edward Lowassa alipokea wito wa kumtaka aonane na DCI leo saa nne bila kukosa.
0 comments:
Post a Comment