Tuesday 27 June 2017

JAY Z AFANYA KUFURU


Huku Beyonce akiwa amejifungua salama na kukaa hospitalini kwa muda wa wiki moja na nusu, hatimaye mwanamama huyo na watoto wake mapacha, wa kiume na kike wameruhusiwa kutoka hospitalini.
Mjengo wenyewe
Habari zaidi kutoka katika ardhi ya US inatutonya kwamba baada ya watatu hao kuruhusiwa kutoka hospitalini, mumewe, Jay Z alikwishaandaa mjengo wa kupanga wa maana uliopo Malibu ambapo watatakiwa kulipia dola 400,000 (zaidi ya milioni 900) kwa mwezi tu.
Mjengo huo wa maana upo karibu na Bahari ya Pasifiki ambapo watapata muda wa kuangalia meli na watu wakila bata lakini pia mjengo una uwanja mdogo wa ndege. Mjengo una hekari 6.3, si hiyo tu, bado mtu mzima Jay Z anaendelea kusaka mjengo mwingine wa kununua huko L.A (Los Angeles).
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive