Friday 30 June 2017

JOSE MOURNHO AONESHA JEURI YA PESA


Kocha wa Manchester United, Jose Mourinho.
HABARI kuwa kiungo wa Chelsea Nemanja Matic anatarajiwa kusa­jiliwa na Kocha Jose Mourinho ndani ya Manchester United kwa dau nono siyo jambo geni kwa kocha huyo raia wa Ureno.
Mourinho hajawahi kuwa na aibu katika suala la matumizi ya fedha za kusajili kwake suala la kuwataka mabosi wake kumwaga fedha nyingi kumpata mchezaji anayemtaka siyo kitu kigumu kwa kuwa amekuwa ak­ifanya hivyo kisha mtihani unabaki kwake kuhakikisha anatwaa mataji.
Kiungo wa Chelsea, Nemanja Matic.
Tabia hiyo ameifanya kote aliko­pita iwe ni Porto, Chelsea, Inter, Real Madrid, Chelsea na sasa anaifanya akiwa ndani ya Mashetani Wekun­du.
Inaelezwa kuwa Matic anaweza kusajiliwa kwa pauni milioni 35, dau ambalo linaonekana ni nono.
Kutokana na hali hiyo, tujikum­bushe wachezaji wanaoweza kuun­da kikosi kwa kila nafasi waliosajiliwa kwa gharama kubwa na kocha huyo.
Kipa Asmir Begovic, Chelsea Pauni 8m (2015)
Alisajiliwa aki­tokea Stoke City, bahati nzuri k w a Mourinho katika nafasi hii ni kuwa makipa wengi aliowaku­ta kwenye timu alizofundi­sha walikuwa na uwezo mkubwa, h i v y o h a k u ­t u m i a gharama kubwa kusajili mbadala.
Baadhi ya majembe aliy­oyakuta ni Petr Cech, Iker Casillas na David De Gea.
Beki wa kulia Paulo Ferreira, Chel­sea Pauni 13.2m (2004)
A l i k u w a mmoja wa ma­beki hodari wa ko­cha huyo amb a y e a l i f a n y a kazi nzuri alipokuwa Chelsea. Kwenye nafasi hii pia hajatumia fed­ha nyingi kwa kuwa huyu alimsajili miaka 13 iliyopita.
Beki wa kati Eric Bailly, Manchester United Pauni 30m (2016)
Aliposajiliwa jina lake ha­likuwa maarufu sana, lakini kwa sasa watu wote wa soka wa England na Ulaya wan­amjua vizuri kutokana na kiwango kizuri alichokionye­sha ndani ya msimu mmoja.
Beki wa kati Victor Lindelof, Man­chester United Pauni 31m (2017).
Ilionekana kama dau al­ilosajiliwa ni kubwa kuliko jina lake lakini ameweza kui­shi ndani ya thamani aliyo­nayo, ndiye chaguo la kwan­za la kocha huyo hadi sasa, kilichomrudisha nyuma ni kuwa na majeraha tu.
Beki wa kati Victor Lindelof, Man­chester United Pauni 31m (2017)
Beki mpya kutoka Ben­fica ambaye hajagusa hata nyasi za uwanjani ak­iwa kwenye jezi yake hiyo mpya.
Inaonekana Mourinho anajua anachokihitaji kuto­ka kwake, wengi hawana ufahamu mkubwa juu yake lakini inavyoonekana anaweza kufiti japokuwa hilo ni deni kubwa kwake.

Beki wa kushoto Fabio Coentrao, Real Madrid Pauni 26.5m (2011)
Baada ya kuonyesha uw­ezo mzuri akiwa ndani ya Benfica na katika michuano ya Kombe la Dunia ya 2010, Coentrao aliele­kea Madrid kujiunga na Mreno mwenzake. Bahati mbaya uw­ezo wake ukawa wa kawaida na hakupata mafanikio makubwa kama ilivyotegemewa.
Kiungo wa kulia Willian, Chelsea Pauni 30m (2013)
Ni aina ya wachezaji ambao wanaonekana hawana vipaji vikubwa lakini ni wepesi wa kujifunza na kujituma. Alikuwa mtumishi mwenye kuamini­wa kwa kocha huyo ambaye alikuwa akimtumia katika mechi muhimu kwa kumpa majuku­mu ya kukaba na kushambulia.
Kiungo wa kati Paul Pogba, Manchester United Pauni 89m (2016)
Ukitaja jina la Pogba unataja fedha. Mchezaji ghali zaidi dun­iani ambaye usajili wake ulizua gumzo kutokana na kuonekana kama thamani yake imekuzwa kupitiliza.
Alirejeshwa klabuni hapo baada ya kuon­doka akiwa mdogo, akapewa mzigo mkubwa wa kutakiwa kuishi kwenye tha­mani ya fedha aliy­osajiliwa, amekuwa na msimu mzuri japo kuna wakati alipata wakati mgumu uwanjani.

Kiungo wa kati Luka Modric, Real Madrid Pauni 33m (2012)
Kiungo fundi ambaye usajili wake uli­zua gumzo kutokana na Spurs kusita ku­muuza, aliposajiliwa alionyesha ufundi kwenye kuuchezea mpira na mpaka sasa bado ni tegemeo kwenye kikosi cha kwanza.

Kiungo wa pembeni Henrikh Mkhitaryan, Man United Pauni 26.3m (2016)
Alianza kwa kuwa na maisha magumu kutokana na kutozoea mazingira, mara kadhaa alilaumiwa na kocha wake la­kini baadaye alianza kuzoea mazingira na kucheza soka zuri.
Mshambuliaji Diego Costa, Chelsea Pauni 35m (2014)

Mourinho amekuwa na kawaida ya kuwa na straika mmoja matata am­baye ni tegemeo. Ndiyo ilivyokuwa kwa Costa, alimsajili licha ya kuonekana alikuwa ni mchezaji mkorofi, lakini ali­pata mafanikio na kuwa staa wa Chel­sea.
Mshambuliaji Andriy Shevchenko, Chelsea Pauni 30m (2006)
Alisajiliwa kwa gharama kubwa licha ya kuwa hakuwa chaguo la Mourinho, matokeo yake akawa na maisha magu­mu na mbinu za kocha huyo hazikum­saidia kuamka na kurejesha enzi zake kama ilivyokuwa.
MANCHESTER, England
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive