Jeshi nchini Iraq limethibitisha
kwamba wanamgambo wa dola ya kiislam Islamic State wameulipua msikiti
mkuu wa Al-Nuri ulioko mjini Mosul .
Msikiti huo unaaminika ndimo
kiongozi wa wanamgambo wa IS Abu Bakr al-Baghdadi alitoa hotuba yake
miaka mitatu iliyopita wakati alipokuwa akitangaza "ukhalifa" mpya.
Wakati
hayo yakijiri, wanamgambo hao wa IS wao wanadai kwamba ndege za jeshi
la Marekani ndiyo zilizo zilizousambaratisha msikiti huo.
Mapema leo, Kamanda wa majeshi ya Iraq aliiambia BBC kwamba
walikuwa mita kadhaa kutoka msikitini hapo, walipokuwa katika harakati
zao za kusonga mbele kwenye mapambano lengo likiwa ni kuteka ngome kuu
ya wanamgambo hao wa kiislam wa Is nchini Iraq.
0 comments:
Post a Comment