MCHEZAJI wa zamani wa Simba, Haruna Moshi Boban anatamani kurudi katika timu yake ya zamani ya Simba.
Haruna aliwahi kucheza Simba akiwa na Emmanuel Okwi na Shomary
Kapombe kwa mafanikio makubwa na kupata bahati ya kucheza soka la
kulipwa nje ya Tanzania kabla ya kurejea nchi ambapo kwa sasa hana timu
ya kuichezea katika ligi kuu.
Akizungumza na moja ya vyombo vya habari hapa nchini
mara baada ya mchezo wa michuano ya Sports Extra Ndondo Cup akiitumikia
Faru Jeuri iliyocheza na FC Kauzu, Boban alisema anatamani siku moja
arudi kuichezea Simba kama watamuhitaji.
“Simba imefanya vizuri kuwarejesha kundini wachezaji Emmanuel Okwi na
Shomary Kapombe ni wachezaji wazuri na watawasaidia sana katika msimu
ujao”alisema Boban.
Boban jana aliisaidia timu yake ya Faru Jeuri kuibuka na ushindi wa
bao 1-0 dhidi ya FC Kauzu mchezo uliofanyika Katika Dimba la Kinesi na
kuhudhuriwa na mchezaji wa Tottenham Hotspur , Mkenya Victor Wanyama
ambaye alikuwa mgeni rasmi.
0 comments:
Post a Comment