Friday 20 January 2017

TFF YAITOLEA UVIVU SIMBA JUU YA UJIO WA OKWI

Kumekua na taarifa zinatembea mitandaoni na utani pia wa Mkuu wa idara ya habari kwenye club ya Simba Haji Manara kwamba baada ya Emmanuel Okwi kuvunja mkataba na timu aliyokua anaichezea huko Denmark, anarudi Simba na kocha akiamua atacheza February.
Sasa baada ya kuwepo kwa hizo taarifa, shirikisho la soka Tanzania (TFF) limeongea yafuatayo "Swala la usajili wa mtu mnaemtaja Okwi, Simba inaweza ikamsajili lakini itamtunza tu ama kucheza mechi za kirafiki lakini kucheza ligi kuu au kombe la FA haiwezekani";
"Kucheza ligi kuu au kombe la FA kwa msimu huu December January mpaka May June hachezi, kwenye mpira wa miguu ukikosa utaratibu, kanuni na sheria mpira wa miguu hamna…. tutakua tunafanya mambo ya ovyo ovyo mwanzo mwisho" – TFF
"Utaratibu huo unaozungumzwa na kanuni hiyo vipo Ulaya ambako kuna Treni za umeme na vitu tofauti, kule ni Ulaya na hapa ni Afrika, hapa ni Tanzania…. anaeongoza mpira na mwenye mpira wake Tanzania ni TFF"
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive