Saturday 7 January 2017

SAKATA LA FARU JOHN LILINITISHA-KALA JEREMIAH


RAPA anayetamba na ngoma ya ‘Wana Ndoto’ Kala Jeremiah amesema sakata la Faru John ambalo limeteka hisia za watu wengi kwa sasa  alipolisikia kwa mara ya kwanza, mapigo yake ya moyo yalimdunda hadi akaogopa.

Akipiga stori na Over Ze Weeked Rapa huyo amesema amekuwa   akisikia kashfa mbalimbali za ufisadi  kwa muda mrefu, lakini hili la Faru John limekuwa la aina yake.

“Nimekuwa nikijaribu  kufuatilia ishu hiyo kwa kina ajabu nakutana na habari  zisizo eleweka kila mtu anamaelezo yake, sakata la Faru John linanifanya niamini uwepo wa sakata la Twiga waliyowahi kupandishwa Ndege  na kusafirishwa Ughaibuni kinyamela.

“Naendelea kujiuliza maswali ambayo sijui majibu yake nitayapata wapi, miongoni mwa yale ninayo jiuliza ni je kuna Faru wangapi wanaokufa huko  katika mbuga za wanyama, na je kwanini kutoweka kwa Faru John kuibue gumzo kiasi hicho, huyo Faru alikuwa na kitu gani kikubwa cha ajabu, lakini kubwa kuliko vyote nimetaharuki baada ya kubaini kuwa kumbe Wanyama huwa wanapewa Majina ya Binadamu.” Alisema Kala Jerimiah
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive