Monday 16 January 2017

POLISI WAHAHA KUMKAMATA LOWASSA WADAI KUMLINDA


Jioni ya January 16 2017 ripoti kutoka Geita kanda ya ziwa zilithibitisha kwamba Waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa amekamatwa na Polisi akiwa anakwenda kwenye mkutano wa CHADEMA hukohuko Geita ambapo baada ya kusambaa kwa taarifa hizo na baadae kuachiwa, Polisi Geita imeyasema haya baada ya kuhojiwa na AMPLIFAYA YA CLAUDS..
1: ‘Hatukumkamata Edward Lowassa bali tulikua tumemshikilia tu huyu bwana, na sababu kubwa kabisa za kuwa nae ni swala zima la ulinzi na usalama’ – Kamanda wa Polisi Geita
2: ‘Usalama wa aina gani…… ni usalama wa kwake yeye kama yeye lakini pia na jamii inayomzunguka, hiyo ndio hoja kubwa iliyokua imejitokeza‘
3: ‘Polisi haikuwa na taarifa yoyote ya Edward Lowassa kuelekea kwenye mkutano wa CHADEMA, na wakato tumemshikilia tulikaa nae mpaka tulipomaliza mahojiano yetu na ndipo tulipomruhusu akaendelea na safari yake‘
ndipo polisi wakadai kuwa mpaka wakati ule walipokuwa wakihojiwa tayari Mh. Lowassa alikuwa akashaachiliwa.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive