Mafisa wa taasisi 
iliyochapisha upya kitabu cha kiongozi wa zamani wa Ujerumani Adolf 
Hitler cha Mein Kampf (Mapambano au Mapigano yangu) wamesema mauzo ya 
kitabu hicho yaliongezeka sana tangu kuanza kuuzwa kwa kitabu hicho 
Januari 2016.
Nakala 85,000 za kitabu hicho kilichoandikwa kwa lugha ya Kijerumani zimeuzwa katika kipindi hicho cha mwaka mmoja.
Mkuu wa Taasisi ya Historia ya Kisasa (IfZ) iliyochapisha kitabu hicho Andreas Wirsching amesema mauzo hayo yamewashangaza sana.
Hata hivyo, bado hakijafikia vitabu vingine vilivyouzwa zaidi nchini Ujerumani.
Nakala ya kitabu hicho huuzwa €58 (£49).
Kitabu hicho kinachoangazia sera aliyoifuata Hitler kilikuwa 
mwongozo wa utawala wa Nazi. Hitler, kwenye kitabu hicho, alieleza wazi 
chuki dhidi ya Wayahudi.
Kitabu hicho kilipigwa marufuku baada ya 
Vita Vikuu vya Pili vya Dunia na serikali ya Bavaria, ambayo ilimiliki 
haki za kitabu hicho.
Hii iliwazuia watu kuchapisha au kusambaza kitabu hicho kwa miaka 70.
Kwa
 mujibu wa Sheria Ujerumani, hakimiliki hudumu kwa miaka 70 na baada ya 
kumalizika kwa kipindi hicho, IfZ ya Munich iliweza kuchapisha kitabu 
hicho na kuanza kukiuza Januari mwaka 2016.
Tofauti na vitabu 
vilivyochapishwa wakati wa utawala wa Nazi, nakala za Mein Kampf za IfZ 
zina jalada la rangi nyeupe ambayo haina picha ya Hitler.
Swastika na nembo nyingine za Nazi ni marufuku Ujerumani.
Inakadiriwa kwamba nakala 4,000 za kitabu hicho ziliuzwa Ujerumani mwaka 2016.
Hatua
 ya kuchapisha upya kitabu hicho ilishutumiwa vikali na makundi ya 
Wayahudi, yanayodai kazi za Sanaa za Nazi hazifai kuendelezwa.
source BBC
source BBC







0 comments:
Post a Comment