Wednesday 11 January 2017

CHRIS BROWN NA SOULJA BOY KUZITWANGA MWAKANI


Drama ya pambano la Chris Brown na Soulja Boy inazidi kushika kasi. Imedaiwa kuwa pambano la ngumi la wawili hao lipigwa katika ulingo huko Dubai.

Chanzo kimoja kimeuambia mtandao wa TMZ, wawili hao wamekubali kupigana kwenye pambano hilo ila wanachotaka ni kupata fedha zaidi kupitia kwa watu ambao watataka kuangalia pambano hilo [Pay-Per-View].

Awali pambano hilo lilipangwa kufanyika mjini Las Vegas lakini kutokana na sheria zilizopo katika mji huo kutokana na mapambano kama hayo ndio imesababisha kubadilishwa kwa ratiba hiyo. Hata hivyo imedaiwa kuwa pambano hilo litakuwa ni kwa ajili ya kujitolea na fedha zitakazopatikana zitatolewa kama msaada.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive