Saturday 31 December 2016

ALIKIBA AONGOZA LISTI YA WASANII WALIOBEBA TUZO NYINGI 2016



Tumezoea kuona wasanii wengi wa Tanzania wakinyakua tuzo nje ya nchi kwa kupitia nyimbo walizoshirikishwa(collaboration) lakini hali hiyo imekuwa tofauti kabisa mwaka huu.
Baada ya mfalume wa Bongo fleva Alikiba kunyakua tuza nyingi za nje na ndani bila colabo ya aina yoyote kutoka kwa msanii wa kimataifa hata wa kitaifa.
Alikiba amenyakua tuzo mbalimbali ikiwemo ile aliyochukua mikononi mwa msanii maarufu wa Nigeria, wizkid ambayo ni MTV EMA, katika kipengele cha Best African Act.
Wizkid alietamba kwa kibao chake cha Oalegoba ambaye alipewa tuzo hiyo kimakosa na hatimae ikabidi bodi ya uwandaaji wa tuzo za MTV Ema za Afrika kumuomba radha alikiba na kumkabidhi tuzo hiyo.
Tuzo nyingine alizochukua Alikiba ni Kenya Coast Music Awards,Celebrity Player Awards,Afsa Award Supdates,EATV Awards 2016,Tz Insta Awards na nyinginezo nyingi.
Alikiba kupitia akauti yake ya Instagram alitoa pongezi zake za dhati kwa mashabiki waliomuwezesha kunyakua tuza hizo na kudai kuwa ataendelea kunyakua tuzo nyingi kwani anaamini uwezo anao.
“Nawashukuru sana kwa kuniwezesha kushinda tuzo nyingi ndani ya mwaka huu am so proud of you na nitakuwa hivyo siku zote” Alisema mfalume wa bongofleva Alikiba.
Alikiba ambaye leo atakuwa Nairobi, nchini Kenya kwa ajili ya kupiga shoo ya funga Mwaka alimaliza kwa kuwaribisha mashabiki wake kwenye shoo na kubainisha kuwa kama wataweza kufika huko atafurahi sana.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive