Monday, 31 October 2016

WAKATI TANZANIA TUNAFIKIRIA MITA 100 NIGERIA WANAFIKIRIA MITA 10,000


Kichwa cha habari kinaweza kikakuchanganya ila ukweli ni kwamba muziki wa Tanzania unasifiwa umekuwa lakini bado wanaofanya vizuri hawafikirii kukua kimataifa zaidi, baada ya kuliteka soka la Afrika ndio inaonekana kazi imeisha.best-new-acts-of-the-year

Wengi wanaweza kunishushua na kusema mbona Diamond anakinukisha kinomanoma kimataifa ? Ukweli unabaki kuwa  hata mawazo yake yanabaki kuwa Afrika ingawaje katika mahojiano mengi husema anataka kulikuza soko la Bongo kimataifa na mipango hiyo kweli ipo na anaonesha. Huku washindani wake nao wakiwa na mawazo mgando mawazo yao yakibaki kugombania ma-fans waliopo Kenya, Uganda na Afrika kwa ujumla. Unadhani kwa aina hii kweli soko letu linakua kimataifa ?. Wakati Afrika Kusini na Nigeria wakituongoza kimuziki kwa miaka mingi  lakini miaka kadhaa tumewaua na sisi kushika namba moja, Afrika Kusini na Nigeria sasa wamerudisha enzi zao, kwani tayari wenzetu wanawaza mbali zaidi.diamond-kiba

NIGERIA WAKOJE ?

Baada ya kuona Tanzania tumekuja vizuri kimuziki, walichokifanya kutengeneza urafiki na nyota wa Tanzania ili wazidi kupenya zaidi na waliweza kufanya hivyo, mfano mzuri Patoranking alikuja Tanzania mwaka 2013 alipiga show ya Fiesta na Waje hivi sasa anachukua wimbo bora wa mwaka na kweli ulistahili.wizkid-tiwa-savage-and-davido-e1411489505467

KWANINI NIGERIA WANAWAZA MITA 10,000 ?

Tayari wameshatwaa ndoo za Afrika kimuziki na wameshafanya makuu, sasa hivi tayari wamewatanguliza wasanii wao kimataifa ili wakaliteke soko hilo akitumwa Davido, Wizkid  na Tiwa Savage huku Davido akisaini na Sony Music na tumeona kazi alizozitoa uzuri wake ameanza na albumu, ngoma ambayo amemshirikisha Tinashe ‘Haw long’  na sasa anatarajia kutoa ngoma nyingine katika albumu hiyo inaitwa ‘For you’  ngoma hizi  tayari zimetusua huku Tiwa Savage akisainiwa na Roc Nation na tayari ametoa ngoma kali  kama Buy Signal.2face-idibia

tuface-and-nino

Unadhani kwa namna hii na jinsi ngoma zao wanavyozipeleka hawafiki mbali ? Bado sijamtaja mnyama mmoja anayeitwa Wizkid Ayo huyu tayari kashapenyesha ngoma zake mbele kwani tayari zimeshakaa katika mstari mzuri. Hivyo Bongo fikirieni upya bila hivyo mtabaki kugombania mashabiki hadi mchoke. Kumbuka aliyeutambulisha vyema muziki wao Nigeria ni  2baba Idibia yeye ndiye aliyebutua kopo la kombolela la Nigeria hadi leo wamefanikiwa. 

SOURCE: MTEMBEZI                                                                                                                         

Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive