Saturday, 3 September 2016

SUMAYE KWENDA MAHAKAMANI KUDAI HAKI YAKE


By Denis Massawe

HATIMAYE Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye, ameamua kukimbilia mahakamani kutafuta haki ya shamba lake la heka 33 lililopo Mji Mpya eneo la Mabwepande, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam, ambalo limevamiwa na wananchi waliogawana viwanja na kujenga makazi.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Sumaye alisema mara baada ya tatizo hilo kutokea na kutumia njia za majadiliano bila mafanikio, ameamua kufungua kesi ili kutafuta haki.Alisema kesi hiyo imefunguliwa na wakili wake na tayari hati ya kuitwa mahakamani wahusika imeshapelekwa kwao.

Mwishoni mwa mwaka jana  wananchi, wakiwamo waliobomolewa nyumba zao katika mabonde ya Mkwajuni na Msimbazi wilayani Kinondoni, wakijikatia maeneo kwa ajili ya viwanja vya makazi mapya.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive