Saturday, 3 September 2016

MKE WA TRUMP ADAI FIDIA KWA WALIOMZUSHIA UKAHABA

Tokeo la picha la MKE WA TRUMP

Gazeti la Daily Mail la Uingereza pamoja na blog moja ya Marekani zimeshtakiwa na mke wa Donald Trump Melania Trump kwa kumchafua kuwa aliwahi kuwa kahaba miaka ya 1990 na akitaka wamlipe kiasi cha $150 milioni.

Wakili wa mama huyo Charles Harder alisema washtakiwa wote kwa pamoja walitoa tuhuma kadha wa kadha kuhusu Melania ambazo ni za uongo kwa asilimia mia moja na zenye lengo la kumharibia mwanamke huyo ambaye mume wake atapeperusha bendera ya Chama cha Republican katika Uchaguzi Mkuu wa Marekani.

Gazeti hilo la Uingereza lilitoa taarifa kuwa inawezekana Melania Trump aliwahi kuhudumu kama kahaba kwa muda alipokuwa jijini New York na pia likieleza kuwa uhusiano wake na mumewe Donald Trump ulianza mapema  kuliko inavyoelezwa sasa, huku mwanablog wa Marekani naye akieleza kuwa Melania ana hofu sana kuhusu maisha yake ya zamani kuwekwa hadharani hususani wakati huu ambapo mume wake anagombea urais wa taifa hilo lenye uchumi mkubwa zaidi duniani.

Madai hayo ya Gazeti la Daily Maily pamoja na blog hiyo ya Marekani yanakanushwa vibaya na Melania Trump na kwa kupitia mwanasheria wake Charles Harder ameomba vyombo hivyo vya habari kumlipa kiasi cha $150M na kubadilisha taarifa zao kitu ambacho kilitekelezwa na vyombo hivyo vya habari lakini suala la kulipwa bado halijaidhinishwa.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive