Thursday, 11 August 2016

Tume yatuma waraka mnzito kwa jeshi la polisi



TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imekishauri Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kusitisha maandamano yake ili kutoa nafasi kwa mahakama kufanya kazi yake kwa umakini bila shinikizo la muda kati ya sasa na Septemba mosi mwaka huu.

Aidha, imelishauri jeshi la Polisi kutotumia neno ‘tutawashughulikia wote watakaokaidi amri’ kwa kuwa imeona maneno hayo yanaweza kusababisha matumizi mabaya ya mamlaka ya jeshi hilo.bahame-Nyanduga 

Katika hatua nyingine, Mahakama Kuu imetupilia mbali maombi ya wadhamini wa Chadema ya kupinga amri iliyotolewa na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali (IGP) Ernest Mangu ya kupiga marufuku mikutano ya kisiasa kwa muda usiojulikana.

Mwenyekiti wa THBUB, Bahame Nyanduga aliyasema hayo jana Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumalizika kwa mkutano uliohudhuriwa na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji na washauri wake pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Demokrasia Tanzania (TCD), Daniel Loya.

Nyanduga alisema Tume iliandaa mkutano huo ili kuzungumzia tamko la jeshi la Polisi la Juni 7, mwaka huu la kuzuia mikutano na maandamano ya vyama vya siasa isiyo ya kiutendaji na tamko la Chadema kuhusu Operesheni ya Umoja wa Kupambana na Udikteta Tanzania (UKUTA) na mikutano wanayopanga kufanya Septemba mosi, mwaka huu.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive