
Beki huyo mwenye umri wa miaka 22 anakuwa mchezaji wa nane kusajiliwa na kocha mpya wa Man City Pep Guardiola, Stones amesaini mkataba wa miaka sita Man City ila dakika kadhaa kabla ya kutangazwa usajili wake. jina lake lilionekana katika list ya wachezaji wa Man City watakaocheza UEFA.

Stori kutoka BBC Sports inaeleza kuwa Stones atakuwa beki wa pili duniani kuuzwa kwa bei ghali, kama utakuwa unakumbuka vizuri Everton msimu uliopita walikataa ofa ya pound milioni 40 kutoka Chelsea ili wamuachie staa huyo ajiunge na miamba ya Stamford Bridge.
0 comments:
Post a Comment