Tuesday 26 September 2017

MTIBWA WAITUMIA YANGA SALAMU

Vicent Andrew 'Dante' (kushoto) akipiga story na Henry Joseph (jezi namba sita) wakati timu zao zilipocheza mechi ya kirafiki kabla ya kuanza kwa msimu uliuopita (2016/2017)
Timu ya Mtibwa Sugar inaongoza ligi ikiwa na pointi 10, lakini baadhi ya mashabiki na wadau wa soka wamekuwa wakiibeza timu hiyo kuwa wamewashikia nafasi baadhi ya vilabu.
ShaffihDauda.co.tz imemtafuta kocha mkuu wa timu hiyo Zuber Katwila ambaye amesema, wanaoibeza timu yake kuwa wameshika nafasi za watu wasubiri wataona kitakachotokea.
“Mimi mwenyewe nimekuwa nikizisikia hizo taarifa watu wakitubeza lakini wanatakiwa watambue kuwa hii ligi haina mwenyewe, kila timu inaweza kuwa bingwa kwa hiyo kama wataendelea kutubeza bila kufanya vizuri wataona kitakachotokea,” Katwila.
Akizungumzia mchezo wao dhidi ya Yanga unaotarajiwa kupigwa Jumamosi Uhuru, amesema anafanya maandalizi na kikosi chake kama mechi zingine za ligi huku akiongeza mbinu za kumfanya atoke na ushindi.
“Ni mechi ngumu ambayo inaweza kutupandisha ama kutushusha kutokana na pointi zetu zilivyo, lakini mimi na wenzangu tunakiandaa kikosi vizuri kama mechi zingine, tumerudi Manungu kwa ajili ya maandalizi zaidi na ndio maana hatujaweka kambi Dar tunataka utulivu,”.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive