Mshambulizi mpya wa Simba aria wa Ghana, Nicholas Gyan amesema yuko tayari kubadili uraia na kuwa Mtanzania.
Gyan
ambaye amejiunga na Simba akitokea katika klabu ya Ligi Kuu Ghana ya
Ebusua Dwarfs, amesema anatamani kuichezea timu ya taifa na ndoto yake
imekuwa ni kucheza timu ya taifa ya Ghana, Black Stars bila ya
mafanikio.
Gyan
ameuambia mtandao mmoja wa Ghana kwamba kama atapewa nafasi ya kubadili
uraia aicheze Tanzania ‘Taifa Stars, yuko tayari kufanya hivyo.
“Kama
nilifunga mabao 11, hata nafasi ya kuingia timu ya taifa inakuwa ngumu.
Kweli sitaona shida kuhamia kule kwa watakaonipa nafasi,” alisema.
Kabla
ya kuja nchini, Gyan aliyefunga mabao 11 katika ligi ya Ghana alikuwa
sehemu ya kikosi cha timu ya taifa ya Ghana iliyokuwa inajiandaa na
mechi ya kuwania kucheza Chan dhidi ya Burkina Faso.
0 comments:
Post a Comment