Tuesday 18 July 2017

MIILI YA WATU WALIOTOWEKA MWAKA 1994 YAPATIKANA KWENYWE BARAFU USWIZI

The spot where the two bodies were found in glacierHaki miliki ya picha
Kuyeyuka kwa mawe makubwa ya barafu nchini Uswisi kumefichua miili miwili inayoaminika kuwa ya mtu na mkewe waliotoweka miaka 75 iliyopita.
Marcelin na Francine Dumoulin walitoweka wakati walienda kuchunga ng'ombe wao katika milima ya Alps mwaka 1942.
Watu hao walikuwa na watoto saba.
Mtoto wao wa mwisho wa kike ambaye sasa ana umri wa 79, anasema habari hizo zimemletea utulivu na anataka kuwafanyia maziko mema.
"Tulitumia maisha yetu yote kuwatafuta," alisema Marceline Udry-Dumoulin.
Uchunguzi wa DNA unatarajiwa kufanywa.
Polisi wanasema kuwa miili hiyo iligunduliwa wiki iliyopita katika eneo la Tsanfleuron na mfanyakazi kutoka kampuni ya kuteleza kwa barafu ya Glacier 3000.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive