Sunday 30 July 2017

GHASIA ZASHUHUDIWA WAKATI WA KURA VENEZUELA

Venezuelan National Guard motorcyclists take cover after coming under fire during a skirmish in Caracas on July 30, 2017Haki miliki ya picha

Matokeo ya awali yanatarajiwa kufuatia uchaguzi wa wajumbe wa Bunge la Katiba uliofanyika nchini Venezuela kwa ajili ya kuandika Katiba Mpya.
Takriban watu kumi wameripotiwa kuuawa katika siku inayotajwa kuwa ni umwagikaji damu baada ya miezi minne ya machafuko.
Zaidi ya watu mia wamepoteza maisha yao.
Kumekuwa na mapambano kati ya polisi na waandamanaji ambao wanapinga Bunge hilo la Katiba ambapo wamekuwa wakiweka vizuizi barabarani.

Police officer wounded in an explosion in the vicinity of the Altamira Square, in CaracasHaki miliki ya picha

Zoezi hilo liligomewa na vyama vya upinzani vinavyompinga Rais Nicolas Maduro vyenye wabunge wengi katika bunge la Venezuela.
Wanasema anataka kuendelea kungangania madarakani.
Mwandishi wa habari wa BBC nchini Venezuela anasema changamoto kubwa kwa Rais Maduro ni namna atakavyoongoza baada ya kupigwa kwa kura hiyo katika mazingira uhasama.

Opposition activists protest in Caracas, on July 24, 2017 Venezuela's angry opposition is pushing for a boycott of an upcoming vote that it dismisses as a ploy by President Nicolas Maduro to cling to power.Haki miliki ya picha
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive