Friday 6 January 2017

WACHINA WATAPELI BILIONI 136 BAADA YA KUANZISHA BEKI FEKI


Leo January 06 2017 habari iliyoripotiwa na vyombo vya habari vya kimataifa imeeleza kuwa mahakama mjini Nanjing, China, imewafunga jela wanaume wawili waliowatapeli wateja kupitia benki bandia.
Watu hao waliotambuliwa kwa majina Zeng na He, walipatikana na makosa ya kujipatia yuan Dola milioni 63 sawa na takribani  Bil 136.6 kutoka kwa wateja 400, wamefungwa jela miaka tisa. 
Imeelezwa walianzisha chama cha ushirika ambacho ofisi yake ndani zilifanana na za benki moja inayomilikiwa na serikali, walikuwa na madawati na makarani wenye sare zilizofanana na makarani rasmi wa benki ya serikali. Hata stakabadhi za kuweka amana ya pesa kwenye benki zilikuwa sawa na za benki ya serikali.
Ingawa taasisi hiyo ilikuwa na kibali cha kuhudumu kama chama cha ushirika, haikuwa na kibali cha kuhudumu kama benki. Wahudumu waliwavutia wateja kwa kuwaahidi viwango vya juu vya riba kwa pesa walizoweka amana.
fake-bank-in-china-nanjing-mou-village-economic-cooperation-unit-inside-banking-hall
Shughuli haramu za taasisi hiyo ziligunduliwa na mfanyabiashara aliyekuwa ameahidiwa riba ya juu alipodai riba aliyoahidiwa lakini akakosa kulipwa na akatoa taarifa kwa maafisa wa polisi mwaka 2014 na baada ya hapo uchunguzi wa kina ulianzishwa.
Source: BBC
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive