Sunday 22 January 2017

PICHA 5: ZIKIMUONESHA YAHYA JAMMEH ANAVYO IACHA MIPAKA YA GAMBIA


Habari nyingine kubwa kwa Afrika sasa hivi ni Yahya Jammeh kukubali kuachia madaraka ya Urais Gambia baada ya kushindwa na mpinzani wake Adama Barrow kwenye uchaguzi mkuu uliopita.
Jammeh ameondoka kwa Ndege kwenye taifa hilo na hii picha hapa chini inamuonyesha akiwa anaingia kwenye Ndege na akipungiwa mikono ya byebye na baadhi ya Wafuasi wake ikiwa ni muda mfupi baada ya Bendi ya Jeshi kutumbuiza.
Wakati wote huo Jammeh alionekana akiwa na kitabu kitakatifu cha Koran na alitumia mkono huohuo ulichokibeba kuwapungia waliojitokeza uwanja wa ndege kumuaga huku ikiaminika anakwenda Guinea kwa sasa wakati akisubiri kuhamia moja kwa moja kwenda kuishi kwenye taifa jingine.
BBC wameripoti kwamba wakati anaondoka uwanja wa ndege Wafuasi wake na baadhi ya Wanajeshi walionekana kuhuzunika na hata wengine kutokwa machozi lakini mitaani wengi wamefurahia kuondoka kwake akiwa ni Rais wa kwanza wa Gambia kuachia madaraka kwa amani toka ilipopata Uhuru mwaka 1965.
Yahya ambaye ameiongoza nchi hiyo kwa miaka 22, saa chache baada ya matokeo kutangazwa alikubali kushindwa lakini baadae akabadili mawazo na kusema amehujumiwa na kwamba yeye ndio mshindi hivyo akaendelea kung’ang’ania madaraka.
Jammeh akiwa kwenye Ndege akiondoka Gambia
Baada ya kuendelea kung’ang’ania Mataifa mbalimbali ya Afrika yalifanya mazungumzo na ECOWAS wakamtaka aachie madaraka ambapo saa kadhaa zilizopita kupitia Television ya taifa akatangaza kukubali kuachia madaraka kwa amani na asingependa kuona umwagaji damu unatokea.
Umoja wa nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS) ulimuamuru Jammeh kuachia madaraka kabla ya saa sita mchana lakini mwenyewe akaomba aachie madaraka ifikapo saa kumi jioni na kweli ametekeleza.
Picha nyingine ikimuonyesha akiwa ndani ya Ndege tayari kwa kuondoka
Gambia ni miongoni mwa mataifa madogo Afrika ambapo mpaka mwaka 2013 sensa ilikua inasema idadi ya watu ni milioni moja na laki nane na maamuzi ya Jammeh kuachia madaraka yalitangazwa baada ya mazungumzo na Marais wa Mauritania na Guine.
Kwenye mji mkuu baadhi ya Raia wa Gambia wameanza kusherehekea kuondoka kwa Jammeh.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive