Sunday 8 January 2017

MGOMBEA UBUNGE MBAGALA AKWAMA MAHAKAMA YA RUFAA


Dar es Salaam. Mahakama ya Rufaa imetupilia mbali maombi ya marejeo ya aliyekuwa mgombea ubunge katika Jimbo la Mbagala kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, kupitia CUF, Kondo Bungo.

Kondo alifungua maombi ya marejeo mahakamani hapo akipinga uamuzi wa Mahakama Kuu kuwaondoa mashahidi wake watatu katika orodha kwenye kesi yake ya kupinga matokeo ya ubunge wa jimbo hilo, kutokana na viapo vyao kuwa na kasoro za kisheria.

Mahakama ya Rufaa katika uamuzi wake imetupilia mbali maombi hayo, baada ya kukubaliana na hoja za pingamizi lililowekwa na wajibu maombi, kuwa hayana mashiko kwani yanakiuka sheria kwa kuwa wametumia kifungu ambacho kinazuia kukata rufaa na kuomba marejeo kwa mambo ambayo ni ya uamuzi usiomaliza shauri mahakamani.

Kwa uamuzi huo, sasa kesi hiyo inasubiri kupangiwa tarehe ya kuendelea kusikilizwa mashahidi wengine wa mdai katika Mahakama Kuu.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive