Sunday, 28 August 2016

JPM - BINADAMU WOTE NI WAMOJA



RAIS John Magufuli amesema kwamba binadamu wanapaswa kuwa wamoja hata kama wana tofauti mbalimbali zikiwamo za kimadhehebu ya dini, siasa na kanda, huku akiwaomba viongozi wa dini kuendeleza juhudi zao za kuliombea taifa na kuwaunganisha wananchi licha ya tofauti walizo nazo.

Dk Magufuli alitoa kauli hiyo jana baada ya kumalizika kwa Misa Takatifu ya kuadhimisha Jubilee ya miaka 50 ya Ndoa ya Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa na mkewe, Anna iliyofanyika kwenye Kanisa la Mtakatifu Petro lililopo Oysterbay jijini Dar es Salaam jana.1Hafla ya Jubilei hiyo ilifanyika nyakati za mchana kwenye Ukumbi wa Kardinali Rugambwa, uliopo kando ya Kanisa la Mtakatifu Petro-Oysterbay na ilitanguliwa na Misa ya shukrani, iliyofanyika katika kanisa hilo majira ya asubuhi.

Jubilei hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Rais Magufuli na mkewe, Mama Janeth , Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete, Rais mstaafu wa Awamu ya Sita wa Zanzibar, Dk Amani Abeid Karume, Mke wa Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere, mawaziri wakuu wastaafu Cleopa Msuya, Dk Salim Ahmed Salim, Jaji Joseph Warioba na Edward Lowassa.

Misa Takatifu ya Shukrani iliongozwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Arusha, Askofu Josephat Lebulu na kuhudhuriwa na maaskofu na maaskofu wakuu saba, akiwemo Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive