Saturday, 13 August 2016

CHADEMA WAGAWA BENDERA NA JEZI KWA AJILI YA UKUTA



CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Pwani kimeanza kugawa vifaa zikiwemo bendera kwa ajili maandalazi ya Umoja wa Kupinga Udikteta ( Ukuta) ambayo yanatarajia kufanyika Septemba mosi mwaka huu.

NGUO ZA CHADEMA

 Katibu wa Kanda ya Pwani wa Chadema, Casimir Mabina, alisema kuwa bendera hizo zitaanza kupeperushwa kuanzia kesho kutwa kwa ajili ya kuunga mkono azimio la Kamati Kuu ya kufanyika oparesheni Ukuta.Alisema oparesheni Ukuta ni lazima ifanyike nchi nzima na kwamba hawako tayari kuona ukandamizaji wa demokrasia unaoendelea kufanywa na serikali ya awamu ya tano ambayo imeonyesha viashiria vya utawala wa kidikteta.

“Tumeona jinsi Rais alivyopiga marufuku wapinzani kukutana kwenye mikutano ya hadhara huku akiwatishia kuwa wakikaidi atawashughulikia na kweli amewaamuru polisi watekeleze amri hiyo ya kuwakamata viongozi wa Chadema na kuwafungulia mashtaka,” alisema

CREDIT-NIPASHE

Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive