Thursday, 11 August 2016

JE MTOTO WA OBAMA ANAFUATA NYAYO ZA BABA YAKE?



Malia-Obama-Caught-On-Camera-Smoking-Weed

Katika moja ya hotuba zake Rais Obama mwaka 2014 alizungumza kuhusu suala la uvutaji wa bangi ambapo alisema kuvuta bangi ni salama zaidi kuliko kunywa pombe lakini akawasisitizia mabinti zake kwamba hilo sio wazo zuri pia ambapo kwa mujibu wa gazeti la The Mirror, limewahi kumuandika Obama akieleza kuwa anaamini uvutaji bangi hauna madhara au athari za hatari kwa mtumiaji binafsi.

 

Pia kwa mujibu wa historia imeandikwa kuwa  Rais Obama aliwahi kuvuta bangi  enzi za ujana wake, ambapo amenukuliwa akisema kuwa  “uvutaji sio kitu ambacho nachochea kifanyike, tambua ni upotezaji muda na inaathiri afya, bangi imehalalishwa kwenye miji ya Colorado na Washington kwa kura ya maoni na ilikuwa ni muhimu kwa ajili ya mataifa kumaliza uhalifu wa vijana wadogo wanaotoka kwenye familia zenye asili ya umasikini”.obama-smoking-a-joint

Hivi karibuni familia ya Rais huyo ambaye yuko mbioni kumaliza muda wake imekumbwa na mambo mbalimbali ikiwemo kusambaa kwa video ya mtoto wake Malia Obama akikatika katika moja ya tamasha nchini humo.obama family

Tukio lingine kumuhusu binti huyo ni kuhusishwa na uvutaji wa bangi, Inasadikiwa Malia alivuta sigara hiyo ‘haramu’ kwenye tamasha la lollapalooza kwenye Jiji la Chicago, jimbo la Illinois ambalo ni jimbo la nyumbani kwa Rais Obama, Mmoja wa wahudhuriaji wa tamasha hilo Jerrdin Selwyn mwenye umri wa miaka 18 alidai kuwa alimkuta Malia akiwa anavuta ganja na marafiki zake na hakukuwa na shaka ya hilo kwani harufu ya bangi ilikuwa wazi. “Kulikuwa na kijana mmoja pale ambaye alikuwa anavuta na akampasia Malia ambaye alishikilia kama kwa dakika moja kisha akampatia mtu mwingine” alidai binti huyo. Na alidai pia kuwa alikuwa na picha zinazoonesha mtoto huyo wa Rais wa Marekani akivuta bangi hiyo. Malia-Obama_2Matukio hayo ya mtoto huyo wa Rais kinara yanazidi kuichafua familia hiyo kwani wengi waliamini, familia yake ingekuwa mfano wa kuigwa ikizingatiwa kuwa Rais huyo amewahi kutaja madhara ya matumizi ya bangi katika moja ya hotuba zake.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Ads

Blog Archive